SEHEMU YA A: Ufahamu
Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali yanayofuata (alama 5)
Unapotembea mjini, chukua tahadhari kubwa sana. Kuna matapeli wanaohadaa watu mjini. Vile vile matapeli hao hujiweka katika makundi ili kungojea watembezi wanaoonekana wageni. Mara wanapowagundua, wao hunasa pesa, simu na vitu vingine na kukimbia navyo. Pia kuna wale hutumia maneno matamu. Wao hukuandama na ukifika kichorochoroni watakupora na kukimbia. Wengine watakupiga na kukuacha umeumia. Iwapo unataka msaada wowote, basi mtafute bawabu au askari akusaidie. Usijiingize kwenye shida tupu bure.
Eleza maana ya neno wanaohadaa. _______________________