Soma habari hii kisha ujibu maswali yafuatayo.
Hapo zamani za kale wanyama wote ambao hula nyasi na majani waliiishi pamoja. Waalishi katika msitu na walikuwa na afya njema.
Wanyama hawa walianza kuzaana na kuwa wengi. Miti nayo ikaanza kuwa michache na mvua kupungua . Wanyama walikosa chakula na hawakujua wafanye nini.
Ndovu alisema wapande miti kwa sababu miti italeta mvua, mvua nayo italeta majani mengi na nyasi. Wanyama walikubaliana kupanda miti kumi mwezi wa Januari. Walichota maji na kunyunyizia miti kwa sababu ya kiangazi. Walipanda miti mitano Februari.
Mvua ilinyesha Machi na wanyama wakapanda miti ishirini. Mwezi wa Aprili, wakapanda miti ishirini na mmoja. Mei na Juni miti kumi na sita. Julai miti mitano, Agosti na Septemba hawakupanda miti yoyote. Oktoba na Novemba wakapanda ishirini na Desemba miti miwili. Mwaka huo wakapanda miti tisini na tisa. Waliendelea hivyo kila mwaka miti ikaongezeka, nyasi na majani vivyo hivyo. Mvua pia ikaendela kunyesha.
Wanyama walikuwa wanakula __________________ na __________________