wayground logo

Free Printable Worksheets

NEW

Font size

S
M
L
XL
Worksheets

Aina za maneno

Total questions: 16

Worksheet time: 5mins

Name
Class
Date
1.

Sentensi gani kati ya hizi haina nomino?

a)

Mama yangu ni mpishi hodari.

b)

Alimpeleka hospitalini.

c)

Mtumishi wa serikali amefika.

d)

Lini Mwalimu atasahihisha mitihani?

2.

Nomino ni nini?

a)

Majina ya watu.

b)

Majina ya watu, wanyama na vitu vyote.

c)

Majina yanayotoa habari zaidi kuhusu wanyama.

d)

Majibu yote si sahihi.

3.

_________________ amefika shuleni. (Chagua jibu lisilo sahihi)

a)

Mwewe

b)

Mwalimu

c)

Mbuzi

d)

Kiti

e)

Bawabu

4.

___mekula chakula kilichobaki. (Chagua kiwakilishi mwafaka)

a)

Zi

b)

Ki

c)

Wa

d)

Ya

5.

Yafuatayo ni aina ya maneno isipokuwa moja.

a)

Vivumishi

b)

Viwakilishi

c)

Viundaji

d)

Vitenzi

e)

Nomino

6.

Mto ni aina gani ya neno?

a)

Nomino

b)

Kitenzi

c)

Kiwakilishi

d)

Kielezi

7.

Mama alimpata mtoto amelala kitandani. (aina gani ya neno lililopigiwa mstari?)

a)

Kitenzi

b)

Kielezi

c)

Kivumishi

d)

Nomino

8.

Kielezi ni nini?

a)

Jina la kitu, watu au mahali.

b)

Neno linalotaja kitu.

c)

Neno linalofafanua kitendo fulani.

d)

Majibu yote ni sahihi.

9.

Sentensi gani sio sahihi?

a)

Aliyekuwa waziri wa Afya amefariki.

b)

Amekuja nyumbani.

c)

Amekuja mtoto nyumbani.

d)

zote ni sahihi.

10.

Mwanaharamia __________________ mashua. (Jaza nafasi kwa kitenzi sahihi.)

a)

kilikamata

b)

Yalikamata

c)

Amekamata

d)

walikamata

11.

Alifungua lango asubuhi. (Neno gani limepigiwa mstari)

a)

Kiwakiishi

b)

Kielezi

c)

Kivumishi

d)

Kitenzi

12.

Kivumishi ni nini?

a)

Neno linalotoa habari zaidi kuhusu nomino

b)

Neno lenye maana sawa na nomino.

c)

Majina ya vitendo vya watu

d)

Neno linalojisimamia.

13.

Viwakilishi _______________________ nomino katika sentensi. (Jibu ipi sio sahihi?)

a)

huwakilisha

b)

haviwi pamoja na

c)

vinakuwa pamoja na

d)

vinasimama badala ya

14.

__________ninapenda kuogelea.

a)

Mimi

b)

Yeye

c)

Mtoto

d)

Yule

15.

Katibu yule ni mrefu. (chagua kivumishi)

a)

Katibu

b)

yule

c)

ni

d)

mrefu

16.

Duma amemkimbiza na kumkamata Swara mbugani. (Chagua kielezi)

a)

Swara

b)

amemkimbiza

c)

Duma

d)

Mbugani.