NEW
Font size
WorksheetsKISWAHILI
Total questions: 12
Worksheet time: 6mins
Ni kipi miongoni mwa vifuatavyo kisichotumika jikoni?
Chano
Fyekeo
Buli
Bilauri
Jua huchomoza upande wa __________.
Magharibi
Kaskazini
Kusini
Mashariki
Daftari la kuandikia lina umbo gani?
Mche
Kopa
Mstatili
Mraba
Mtoto wa mjukuu wangu nitamwitaje?
Mpwa
kitukuu
Kilembwe
Kinying'inya
Mnyama wa msituni anayefanana na nguruwe ni ________
nyati
kifaru
ngiri
swara
Anayemsaidia daktari hospitalini kwa kuwapa wagonjwa dawa na kuhakikisha wamekula anaitwa _____________.
tabibu
mchuuzi
msusi
mwuguzi
Ni nini hutumika pamoja na kinu kutwangia vitu jikoni?
Mche
Mbuzi
Mchi
Buli
Ni vazi lipi huvaliwa na wanawake pekee?
Kanchiri
Suruali
Koti
Kizibao
Rangi ya juu ya upinde wa mvua ni __________ .
machungwa
samawati
nyekundu
kijani
Yupi kati ya wanyama wafuatao ni tofauti na wengine?
Sokwe
Kima
Swara
Tumbiri
Samaki ni kwa maji kama vile ndege ni kwa ___________ .
kombe
kizimba
mzinga
kiota
- Kati ya shughuli hizi, ni ipi huja ya kwanza?
Kupanda
Kulima
Kupalilia
Kuvuna
