wayground logo

Free Printable Worksheets

NEW

Font size

S
M
L
XL
Worksheets

WANYAMA WA MAJINI

Total questions: 21

Worksheet time: 7mins

Name
Class
Date
1.

Samaki mkubwa kuliko samaki wote bararini,mwenye ngozi ngumu ya kijivu, meno makubwa makali anayekula watu.

a)

PAPA

b)

NYANGUMI

c)

NGUVA

d)

PWEZA

2.

Mnyama mkubwa wa bahari mwenye umbo kama la samaki, mwenye mafuta mengi na hunyonyesha kama wanyama wengi.

a)

TAA

b)

NYANGUMI

c)

DAGAA

d)

KIBOKO

3.

Samaki wa rangi ya fedha wenye umbo dogo sana ambao hawawezi kukua zaidi.

a)

PAPA

b)

MKUNGA

c)

SANGARA

d)

DAGAA

4.

Kidudu kinachoishi ndani ya kombe.

a)

PWEZA

b)

KOCHE

c)

CHAZA

d)

SANGARA

5.

kiumbe wa baharini mwenye gamba gumu jeusi, mwili mrefu uliogawanyika sehemu sehemu, miguu minane na mikono miwili yenye makucha ya kushikia ambaye anapopikwa gamba lake hubadilika na kuwa jekundu.

a)

KOCHE

b)

CHURA

c)

KIBOKO

d)

CHAZA

6.

samaki mkubwa wa baharini mwenye umbo bapa na mkia mwembamba mrefu.

a)

MKUNGA

b)

DAGAA

c)

KAMBA

d)

TAA

7.

samaki mwenbamba mrefu mwenye umbo la nyoka ambaye ni mweusi au wa kijivu, kahawia ay mabatobato.

a)

PAPA

b)

NGUVA

c)

MKUNGA

d)

MAMBA

8.

samaki wa maji baridi mwenye kichwa kikubwakigumu cha bapa na masharubu marefu.

a)

KONOKONO

b)

CHURA

c)

TAA

d)

KAMBARE

9.

Mnyama wa baharini mwenye mikia minane.

a)

PWEZA

b)

NGUVA

c)

KIBOKO

d)

KAMBA

10.

Mnyama wa jamii ya kenge lakini mkubwa zaidi ambaye ana magamba na huishi kwenye maji.

a)

POMBOO

b)

MAMBA

c)

KIBOKO

d)

NYANGUMI

11.

Mnyama mkubwa anayeishi mitoni au katika maziwa na mabwawa mwenye masikio madogo, meno makubwa na mapana na pua pana yenye mianzi mipana.

a)

KIBOBO

b)

NYANGUMI

c)

PAPA

d)

MAMBA

12.

Mnyama mdogo wa baharini mwenye magamba laini na miguu mingi ambayr huliwa.

a)

KAMBA

b)

TAA

c)

MAMBA

d)

DAGAA

13.

Samaki mkubwa mrefu mwenye kivimbe cha duara na rangi ya kijivu aishiye baharini.

a)

KAMBA

b)

KAMBARE

c)

NGURU

d)

PWEZA

14.

Samaki wa maji baridi, wa jamii ya perege aliye na umbo kubwa na mdomo mpana.

a)

MKUNGA

b)

KONOKONO

c)

PAPA

d)

SANGARA

15.

Mnyama mdogo wa majini mwenye miguu sita au Zaidi na gamba mwilini.

a)

KOCHE

b)

PAPA

c)

PWEZA

d)

KAA

16.

Mnyama wa baharini anayenyonyesha watoto wake mwenya umbo la binadamu

a)

MAMBA

b)

NGUVA

c)

KIBOKO

d)

NYANGUMI

17.

Mnyama wa baharini afananaye kobe.

a)

TAA

b)

KASA

c)

DAGAA

d)

PAPA

18.

Samaki mkubwa wa baharini anayefanana na papa

a)

PWEZA

b)

KIBOKO

c)

POMBOO

d)

NGURU

19.

Mnyama mwenye ngozi laini asiye na mkia

a)

SANGARA

b)

CHAZA

c)

SAMAKI

d)

CHURA

20.

Mnyama mdogo anayeteleza na kutambaa polepole

a)

CHURA

b)

KAMBA

c)

KONOKONO

d)

PWEZA

21.

Kiumbe anayeishi majini mwenye mapezi-fins na mkia

a)

MAMBA

b)

TAA

c)

CHURA

d)

SAMAKI