wayground logo

Free Printable Worksheets

NEW

Font size

S
M
L
XL
Worksheets

KISWAHILI SHAIRI

Total questions: 40

Worksheet time: 40mins

Name
Class
Date
1.

Shairi lililo na vipande vitatu huitwaje?

a)

Utenzi

b)

Ukwapi

c)

Ukawafi

d)

Mathnawi

e)

Ukawafi

2.

Gani kati ya hizi bahari siyo inayotokana na idadi ya vipande?

a)

Ukawafi

b)

Mathnawi

c)

Ukara

d)

Utendi

3.

Shairi lililo na neno maalum katika kila ubeti huitwaje?

a)

Kikai

b)

Mandhuma

c)

Kikwamba

d)

Sabilia

4.

Shairi lililo na kipande kimoja kifupi kuliko kingine huitwaje?

a)

Kikai

b)

Ukara

c)

Ukaraguni

d)

Msuko

5.

Shairi lililo na mshororo mmoja mfupi kuliko mingine huitwaje?

a)

Kikai

b)

Mandhuma

c)

Utenzi

d)

Msuko

6.

Ikiwa hoja kwenye shairi linakamilishwa kwenye kipande kinachofuata katika kila mshororo, shairi hilo hujulikanaje?

a)

Mathnawi

b)

Upindu

c)

Kikwamba

d)

Mandhuma

7.

Ni neno gani lisilo na maana sawa kwa shairi linaloanzishwa na maneno yanayolimaliza?

a)

Upindu

b)

Mkufu

c)

Nyoka

d)

Sabilia

8.

Shairi lililo na bahari zaidi ya moja hujulikana vipi?

a)

Sabilia

b)

Mtiririko

c)

Sakarani

d)

Kikwamba

9.

Shairi lisilo na kibwagizo huitwaje?

a)

Sakarani

b)

Sabilia

c)

Msuko

d)

Mandhuma

10.

Shairi lenye vipande viwili kwa kila mshororo hujulikana vipi?

a)

Mathnawi

b)

Mazda

c)

Ukawafi

d)

Ukara

11.

Shairi lenye urari wa vina huitwaje?

a)

Masivina

b)

Shairi huru

c)

Mtiririko

d)

Ukaraguni

12.

Shairi lisilo na urari wa vina huitwaje?

a)

Shari huru

b)

Kikai

c)

Masivina

d)

Tumbuizo

13.

Shairi lenye kipande kimoja kwa kila mshororo huitwa?

a)

Masivina

b)

Mathnawi

c)

Ukawafi

d)

Utenzi

14.

Shairi lililo na vina vinavyobadilika kutegemea ubeti huitwaje?

a)

Ukaraguni

b)

Ukara

c)

Mtiririko

d)

Sabilia

15.

Shairi ambalo vina vya kipande kimoja hubadilika na vya kipande kingine kubakia vile vile huitwaje?

a)

Ukaraguni

b)

Ukara

c)

Ukwapi

d)

Mathnawi

16.

Shairi lililo na vina vinavyobadilika kutegemea ubeti huitwaje?

a)

Ukaraguni

b)

Ukara

c)

Mtiririko

d)

Sabilia

17.

Gani kati ya hizi siyo idhini ya kishairi?

a)

Tabdila

b)

Mazida

c)

Inkisari

d)

Tarbia

18.

Mshororo wa tatu wa shairi huitwaje?

a)

Mloto

b)

Ukwapi

c)

Mleo

d)

Utao

19.

Shairi lenye vipande vinne huitwaje?

a)

Mavue

b)

Mleo

c)

Ukawafi

d)

Mathnawi

20.

Kipande cha tatu kwenye shairi huitwaje?

a)

Mwandamo

b)

Mavue

c)

Ulingo

d)

Ukwapi

21.

Shairi lisilo na urari wa vina wala mizani ni?

a)

Mavue

b)

Masivina

c)

Shairi huru

d)

Shairi guni

22.

Shairi lenye mizani minane kwa kila kipande ni?

a)

Ukawafi

b)

Tumbuizo

c)

Ukingo

d)

Tathlitha

23.

Kwa kueleza umbo la shairi, kigezo hiki hakizingatiwi. Kipi?

a)

Idadi ya mishororo

b)

Idadi ya vipande

c)

Idadi ya mizani

d)

Kurudiwa kwa kibwagizo

24.

Kutumia misamiati ya jadi ni uhuru gani kwenye shairi?

a)

Lahaja

b)

Utohozi

c)

Tabdila

d)

Ukale

25.

Kufupisha maneno kwenye shairi kwa kutumia king'ong'o ni idhini gani?

a)

Inkisari

b)

Mazda

c)

Lahaja

d)

Ritifaa

26.

Shairi lenye mishororo minne katika kila ubeti huitwaje?

a)

Mavue

b)

Tathlitha

c)

Tarbia

d)

Mathnawi

27.

Shairi ambalo neno la mwisho huanza ubeti unaofuata huitwaje?

a)

Upindu

b)

Nyoka

c)

Zingo

d)

Mkufu

28.

Neno nyuta liko katika ngeli gani?

a)

I-ZI

b)

U-ZI

c)

U-YA

d)

I-I

29.

Neno kitungule linapatikana kwa ngeli gani?

a)

KI-VI

b)

I-ZI

c)

A-WA

d)

I-I

30.

Taja ngeli ya uhubiri

a)

U-YA

b)

U-U

c)

I-ZI

d)

U-ZI

31.

Umoja wa mitume ni?

a)

Mitume

b)

Tume

c)

Mtume

d)

Utume

32.

Gani kati ya hizi siyo sifa bainifu ya sauti /b/?

a)

Kipasuo

b)

Hutamkwa mdomoni

c)

Hafifu

d)

Ghuna

33.

Mbinu ya kifasihi ambayo huhusisha upigaji wa picha akilini huitwaje?

a)

Taharuki

b)

Latifa

c)

Taswira

d)

Takriri

34.

Methali ifuatayo ina mbinu gani ya kifasihi?

Tamaa mbele mauti nyuma.

a)

Taashira

b)

Tanakuzi

c)

Jazanda

d)

Balagha

35.

Wewe ni wembe ni mbinu gani?

a)

Tashhisi

b)

Tashbihi

c)

Istiara

d)

Jazanda

36.

Bainisha mbinu katika kitendawili hiki. Huku ng'o na kule ng'o

a)

Kitendawili

b)

Tanakali ya sauti

c)

Takriri

d)

Tashtiti

37.

Hadithi ambapo mhusika hukabiliwa hali ngumu ya kuamua baina ya mambo mawili au zaidi yanayomkabili huitwaje?

a)

Ngano za mazimwi

b)

Ngano za mtanziko

c)

Mighani

d)

Visasili

38.

Ngano ya majitu huitwaje?

a)

Ngano za mazimwi

b)

Ngano za mtanziko

c)

Mighani

d)

Soga

39.

Andika sentensi hii kwa wingi:

Dereva alipomwona askari, alishusha abiria haraka.

a)

Dereva alipowaona maaskari, aliwashusha maabiria haraka.

b)

Madereva walipowaona askari, waliwashusha abiria haraka.

c)

Madereva walipowaona askari, waliwashusha maabiria haraka.

d)

Dereva alipowaona maaskari, aliwashusha abiria haraka.

40.

Neno gani halipatikani katika ngeli ya LI -YA?

a)

Jembe

b)

Limau

c)

Karatasi

d)

Tunda