wayground logo

Free Printable Worksheets

NEW

Font size

S
M
L
XL
Worksheets

Sarufi:Aina za Maneno

Total questions: 25

Worksheet time: 53mins

Name
Class
Date
1.

Panga maneno haya kama yanavyopatikana katika kamusi


i.Chimba

ii.Chimbua

iii.Chimbo

iv.Chimbia

a)

i,ii,iii,iv

b)

iv,i,iii,ii

c)

i,iv,iii,i

d)

iii,ii,i,iv

2.

Sahihisha sentensi ifuatayo:


Darasani waliopo wanafunzi mna jasho nyingi

a)

Darasa waliopo wanafunzi pana jasho nyingi.

b)

Darasani waliomo wanafunzi mna jasho nyingi.

c)

Darasani waliomo wanafunzi mna jasho jingi.

d)

Darasa walipo wanafunnzi mna jasho mingi

3.

Kunitania anakonitania kunaniudhi sana.Ngeli iliyotumika ni gani?

a)

Ki-Vi

b)

Pa-Ku-Mu

c)

Ku-Ku

d)

I-Zi

4.

Ni sentensi gani sahihi?

a)

Pazia zote zimeanikwa nyasini.

b)

Vyura vyote vilikufa maji yalipokauka.

c)

Mapua ya ng'ombe hayaliki.

d)

Majiko yamewashwa na wajakazi.

5.

Tumia viambishingeli vifaavyo kujaza pengo;


Ndizi hi__ __bivu ni __dogo sana

a)

o;m;n

b)

zi;m;n

c)

li;m;n

d)

le;m;n

6.

Maneno yafuatayo yanapatikana katika ngeli gani?


Uwele,Utete,Ulezi

a)

U-U

b)

U-Ya

c)

U-Zi

d)

U-I

7.

Ngeli ya A-Wa hujumuisha viumbe wenye uhai,nayo ya Pa-Ku-Mu ni ya

a)

Vitenzi

b)

Nomino

c)

Mahali

d)

Wingi

8.

Ni nomino gani ambayo ni ya dhahania?

a)

Maziwa

b)

jozi

c)

mwizi

d)

urembo

9.

Ni kundi lipi lenye nomino za kawaida pekee?

a)

Mlolongo,umati,genge

b)

Mwalimu,mnyama,chakula

c)

mti,Nairobi,Mbwa

d)

Pakashume,Mwekahazina,mwananchi

10.

Kiwakilishi ni neno ambalo husimamia____________

a)

kitenzi

b)

kivumishi

c)

kielezi

d)

nomino

11.

Mpira huu na ule yote ni ya kandanda.


Maneno yaliyopigwa kijistari yametumikaje?

a)

Kimilikishi,kisifa

b)

kivumishi,kiwakilishi

c)

kielezi,kiwakilishi

d)

kisifa,kielezi

12.

Tambua kihusishi:


Wamesimama kando ya barabara wakisubiri gari.

a)

wakisubiri

b)

gari

c)

wamesimama

d)

kando ya

13.

Jaza kwa kihusishi kifaacho zaidi


Ndege wengi hujenga viota_________________mti.

a)

chini ya

b)

juu ya

c)

miongoni mwa

d)

kando ya

14.

Mbona unatembea bila sweta_______________kuna baridi.

a)

ilhali

b)

iwapo

c)

sembuse

d)

na

15.

"Ki" imetumikaje katika sentensi ifuatayo?


Kiendacho kwa mganga hakirudi.

a)

kielezi

b)

masharti

c)

wakati

d)

kiwakilishi

16.

Nitawaona watakapokuja kesho


Viwakilishi vilivyopigwa mstari ni vya

a)

nafsi ya kwanza na ya tatu

b)

nafsi ya pili na ya kwanza

c)

nafsi ya kwanza na ya pili

d)

nafsi ya pili n aya tatu

17.

Tambua kiwakilishi katika sentensi hii


Wengine badoo wanaendeleza ukabila.

a)

bado

b)

wengine

c)

ukabila

d)

wanaendeleza

18.

Mkifika msikitini mtapata babu akiali.

Neno lililopigwa mstari ni ?

a)

kielezi cha namna

b)

Kielezi cha mahali

c)

Kielezi cha idadi

d)

kielezi cha wakati

19.

Mwali amekula maembe mengi sana


Neno lililopigwa mstari ni________________

a)

kielezi

b)

kivumishi

c)

kibadala

d)

kiwakilishi

20.

Kutokana na kitenzi "ogopa" tunapata nomino "mwoga".Kutokana na kitenzi "iba" tunapata nomino___________

a)

mwiba

b)

mwizi

c)

mwibaji

d)

mwibi

21.

Tuliandikiana barua naye.


Kauli gani imetumika?________________________

a)

kutendana

b)

kutendeana

c)

kutenda

d)

kutendeeana

22.

Vitenzi pia huitwa___________________?

a)

nomino

b)

vibadala

c)

visifa

d)

viarifa

23.

Nyambua katika kauli ya kutendesha:


oa;jua;kaa

a)

olesha;juza;ketisha

b)

olesha;juvya;kasha

c)

oza;juvya;kalisha

d)

oza;julisha;kasha

24.

Tumia kiunganishi kifaacho kujazia pengo.


Mwana wa mnyama hufuata amri___________________wa binadamu.

a)

isipo

b)

ila

c)

kaifa

d)

mintarafu

25.

Nitupie mpira huo.


Maana ya sentensi hii ni__________________

a)

Utupe mbali,utupe kwa niaba yangu.

b)

Utupe nilipo,utupe mbali

c)

Utupe kwako,utupe mahali fulani

d)

Utupe kwa niaba yangu,utupe nilipo