WorksheetsKISWAHILI
Total questions: 20
Worksheet time: 20mins
Picha hii ina mmea mchanga. Je, mmea mchanga huitwaje?
mchi
mche
mimea
mparachichi
Andika sentensi ifuatayo kwa umoja?
Mihogo yao imeiva.
mhogo wake umeiva
muhogo wake umeiva
muhogo wao umeiva
muhogo wangu umeiva
Mmea unaozaa kahawa huitwa_______
mche
kahawa
mbuni
mgomba
Ndizi huwa na utamu mwingi. Je, mmea unaozaa ndizi huitwaje?
mndizi
mpera
mpunga
mgomba
Mmea huu huzaa maembe. Wingi wake ni miembe. Umoja wa miembe ni __________
embe
myembe
mwembe
muhogo
Mmea huu huitwa mpunga. Je, unazaa zao gani?
wali
mchele
parachichi
mahindi
Mtu anayeimba mashairi huitwa_____
mshororo
manju
malenga
mghani
Kipofu, mtume, chura, kipepeo na bata ni nomino zinazopatikana katika ngeli ya ________
KI-VI
A-WA
LI-YA
U-I
Nomino darasa, magari, goti, tumbo, daftari na madawati hupatikana katika ngeli gani?
LI-YA
KI-VI
A-WA
U-I
Mshororo unaorudiwarudiwa katika shairi huitwaje?
malenga
kibwagizo
shairi
tarbia
________ni shairi la mishororo minne katika kila ubeti.
tathmina
tarbia
tathlitha
tathnia
Chombo kinachotumiwa kuonyesha pande za dunia huitwa__________
jua
dira
kochi
jokofu
Jua huchomoza kutoka upande wa ___________
kaskazini
kusini
magharibi
mashariki
Bendera ya nchi yetu ina rangi nne. Je, ni rangi gani husimamia ardhi?
nyeusi
nyekundu
kijani kibichi
nyeupe
Maneno yafuatayo huitwaje?
papa-baba
pipi-bibi
koti -goti
kinyume
vitate
visawe
kielezi
Neno lililopigiwa mstari ni mfano wa neno gani ya Kiswahili?
Mayai matano yamevunjika.
kielezi
kivumishi
nomino
kitenzi
Hii ni suruali ya miguu mifupi ambayo hujulikana kama kaptura au _____
kocho
bombo
kamisi
sare
Mavazi haya huvaliwa na wachezaji. Je , yanaitwaje?
sare
jezi
chupi
daluga
Maneno yafuatayo huitwaje?
Ebo!, Lo!, Masalaale!, Aha!, Kumbe!, Huree!, Alhamdulillahi!, Hoyee!
viwakilishi
vihusishi
vihisishi
vielezi
Jaza pengo kwa kutumia kiunganishi kifaacho.
Hakunywa chai _______uji.
lakini
wala
na
pia
