wayground logo

Free Printable Worksheets

Font size

S
M
L
XL
Worksheets

Luka 8-14

Total questions: 17

Worksheet time: 22mins

Name
Class
Date
1.

na wanawake kadha wa kadha ambao walikuwa na pepo wabaya na magonjwa wakaponywa; nao ni Mariamu aitwaye Magdalene aliyetokwa na pepo saba....pamoja na wanawake wengine walikuwa na sifa gani ya ziada?

a)

Walimsihi Yesu akae kwao

b)

Walimhudumia Yesu kwa Mali zao.

c)

Walikuwa wasomi wa sheria

2.

Katika mfano wa mpanzi alioutoa Bwana Yesu, mbegu zinawakilisha au zina tafsiri ya (a)  

3.

Hawa ndio wasikiao, kisha huja Ibilisi akaliondoa hilo neno mioyoni mwao, wasije wakaamini na kuokoka.

a)

Wa kwenye mwamba

b)

Kwenye njia

c)

Kwenye miiba

d)

Udongo mzuri

4.

Na wale wa kwenye mwamba ....?

a)

Husongwa na shughuli na mali na anasa za maisha

b)

Hulipokea neno kwa furaha , wakati wa kujaribiwa hujitenga

c)

Huzaa na kushika mizizi kwa kuwa zipo mwambani

d)

Hilisikia neno la Mungu lakini hawalitendei kazi

5.

Lk 8:51 SUV

[51] Alipofika nyumbani hakuacha mtu kuingia pamoja naye ila Petro, na Yohana, na Yakobo, na babaye yule mtoto na mamaye.

Kwa kutafakari kwako, kwanini Yesu aliamua kuingia na Petro, Yohana, Yakobo pamoja na wazazi wa mtoto pekee?

4 lines
6.

Ilikuwa miaka mingapi kwa mwanamke aliponywa na Yesu aliye kuwa akitokwa na Damu (a)  

7.

Wakafika pwani ya nchi ya (a)   inayoelekea Galilaya. Naye aliposhuka pwani, alikutana na mtu mmoja wa mji ule, mwenye pepo, hakuvaa nguo siku nyingi, wala hakukaa nyumbani, ila makaburini.

8.

Wale mitume kumi na wawili kwa jina mmoja waliitwa?

(a)  

9.

Katika muujiza wa kulisha watu kwa samaki wawili na mikate mitano walikuwa wanaume wangapi?

(a)  

10.

Watu kwa safu ya watu 50

Waliketishwa kula, Kwa samaki wawili na mikate mitano zili g watu na wote walikula na vikapu (a)   vikasalia

11.

Lk 9:23 SUV

[23] Akawaambia wote, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate.

Maneno haya Ina maana gani ?

Tutafakari pamoja..

4 lines
12.

Lk 9:26 SUV

[26] Kwa sababu kila atakayenionea haya mimi na maneno yangu, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wake na wa Baba na wa malaika watakatifu.

Msisitizo hapa ni....?

4 lines
13.

Ukuu wa kweli ni upi, kwa mafundisho ya Bwana Yesu miongoni mwa wanafunzi wake walipo kuwa wakijiuliza nani atakuwa mkuu kati yao?

a)

Kuwa na Imani kiasi cha punje ya haradari..

b)

Kujikana mwenyewe na kubeba msalaba kila siku na kumfuata Yesu.

c)

Kwa kuwa aliye mdogo miongoni mwenu ndiye mkubwa

d)

Atakaye kuingiza nafsi yake kwa ajili ya Yesu na Injili...

14.

Akawageukia, akawakanya. [Akasema, Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.]

Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine.

Haya ni maneno ya Bwana Yesu kwa wanafunzi wake, walipomwambia Yesu aagize moto kuchoma samaria ilipokataa kumkaribisha, tunajifunza nini hapa kwa jibu la Bwana?

a)

Mshahara wa dhambi ni mauti

b)

Kila mtu atabeba mzigo wake mwenyewe baba atauchukua uovo wa mwana.

c)

Roho na nia njema ya wa upendo wa Yesu kwa wanadamu wote.

d)

Mtu asipoong'oka kama mtoto mdogo kamwe haingii ufalmewa Mungu

15.

Ikawa alipokuwa akisema maneno hayo, mwanamke mmoja katika mkutano alipaza sauti yake, akamwambia, Heri tumbo lililokuzaa, na matiti uliyonyonya.

Yesu akajibu....

a)

Heri wenye njaa na kiu ya haki..

b)

Heri wasikiao neno la Mungu na kulishika

c)

Heri wasiochukizwa nami

16.

Taa ya mwili ni jicho; basi jicho lako likiwa safi, mwili wako wote unao mwanga; lakini likiwa bovu, mwili wako nao una giza.

Tqfsiri yake ni ipi?

4 lines
17.

Chachu ya mafarisayo ni (a)