WorksheetsCHEMSHABONGO -1
Total questions: 15
Worksheet time: 8mins
Kipi kati ya hivi si kiungo cha mapishi?
bizari
ndizi
pilipili
kitunguu
Geuza katika wingi: Mkate nilioula ulikuwa mtamu.
Mikate tulizozila zilikuwa tamu.
Mikate niliyoila ilikuwa mitamu.
Mikate tuliyoila ilikuwa tamu.
Mikate tuliyoila ilikuwa mitamu
Mtoto wa chui huitwaje?
shibli
kinegwe
kisui
kiluwiluwi
Mwenye ujuzi wa kusanifisha na kusahihisha makala k.v ya magazeti huitwaje?
mhariri
malenga
tarishi
mhazili
Pesa za matumizi ya kila siku hasa safarini ni _________
marupurupu
masurufu
arbuni
bahashishi
Jina wanaloitana dada yake mume na mke ni ____________
mwamu
umbu
mkoi
wifi
Kamilisha: Shuleni _____________ mna maji.
huku
humu
hapa
mumo
Pazia _______________kwenye dirisha
limening'inia
zimening'inia
imening'inia
umening'inia
Mdudu akaaye kwenye nywele na nguo chafu huitwaje?
chawa
funza
kunguni
kiroboto
Kamilisha methali: Baada ya kisa ______________
faraja
mkasa
kitendo
mkosi
Majira ya mvua ndogondogo huitwaje?
masika
kipupwe
kifuku
vuli
Andika kinyume cha: Mfalme bahili amerudi.
Malkia bahili ameenda.
Malkia karimu hajarudi
Malkia karimu ameenda.
Malkia karimu amerudi.
Mtu anayefanya kazi ya kufua vyuma huitwaje?
sonara
mjumu
mwashi
mhunzi
Maneno haraka,polepole,upesi, sana, chapuchapu ni mfano wa _____________
vivumishi
vielezi
vitawe
viwakilishi
Saruji ni tandiko la farasi. Saruji pia ni ______
simiti
mbolea
hori
changarawe
