wayground logo

Free Printable Worksheets

NEW

Font size

S
M
L
XL
Worksheets

MASWALI

Total questions: 50

Worksheet time: 50mins

Name
Class
Date
1.

Je,nomino mkoba inapatikana katika ngeli gani?

a)

U-U

b)

I-ZI

c)

U-I

d)

U-YA

2.

Jaza pengo.

________ tunapenda kusoma vitabu vya hadithi.

a)

wewe

b)

mimi

c)

sisi

d)

wao

3.

Nyambua kitenzi ogopa katika kauli ya kutendesha.

a)

ogofya

b)

ogopwa

c)

ogopesa

d)

ogopeza

4.

Ukitaka kupima kilo ya sukari utatumia nini?

a)

utepe

b)

rula

c)

mizani

d)

timazi

5.

Ukitaka kumpima mtu nguo utatumia nini?

a)

utepe

b)

mizani

c)

timazi

d)

randa

6.

Tumia amba kwa usahihi.

Mvua _____ hunyesha vizuri huleta manufaa.

a)

ambayo

b)

ambao

c)

ambalo

d)

ambazo

7.

Sentensi ifuatayo iko katika wakati gani?

Sijafika mapema wala sijampata.

a)

uliopo

b)

timilifu

c)

uliopita

d)

ujao

8.

Kanusha: Mgeni wa heshima akifika tutamkaribisha.

a)

Mwenyeji wa heshima akirudi tutamfukuza

b)

Mgeni wa heshima asipofika hatutamkaribisha.

c)

Mgeni wa heshima angefika tungemkaribisha.

d)

Mgeni wa heshima hatafika na hatutamkaribisha.

9.

Chagua nomino ya dhahania.

a)

maji

b)

halaiki

c)

kalamu

d)

ukarimu

10.

Ni tamathali gani ya lugha imetumika katika sentensi ifuatayo?

Akwiri ni wembe masomoni.

a)

nahau

b)

sitiara

c)

tashbihi

d)

methali

11.

Jaza pengo.

Chumbani _________ mna uchafu mwingi.

a)

kwao

b)

mwao

c)

pao

d)

ambapo

12.

Kamilisha methali.

Nia zikiwa moja ____________ .

a)

kilicho juu huja

b)

kuni huwaka

c)

watu wanafanikiwa

d)

kilicho mbali huja.

13.

Shairi la mishororo mitatu katika kila ubeti huitwa_____

a)

tarbia

b)

tathlitha

c)

takmisa

d)

tathmina

14.

Watano wamemaliza kazi ya ziada.

Neno lililopigiwa mstari ni ________

a)

Kivumishi

b)

kiwakilishi

c)

kielezi

d)

kihusishi

15.

Kamilisha maamkizi haya.Shikamoo ni kwa marahaba kama vile waambaje ni kwa________

a)

sina jambo

b)

siambi

c)

sina niambalo

d)

sijambo au salama

16.

Tambua aina za maneno yaliyopigiwa mistari.

Mtoto mzuri amekimbia hadi shuleni.

a)

kivumishi,nomino

b)

kielezi,kivumishi

c)

kivumishi, kielezi

d)

kihusishi,kiwakilishi

17.

Andika kwa ukubwa.

Mti huu ni mkubwa sana.

a)

jiti hili ni kubwa sana.

b)

Majiti haya ni ni makubwa sana.

c)

Kijiti hiki ni kikubwa sana

d)

Miti hii ni mikubwa sana.

18.

Chagua sentensi sahihi.

a)

Watu wasita walikula nyama.

b)

Magari kumi na tatu yalinunuliwa.

c)

Kalamu ya mwalimu ni mzuri.

d)

Viatu vinane vimepigwa rangi.

19.

Ni pambo lipi limeambatanishwa vilivyo?

a)

Sikio-mapete

b)

Mguu-kipini

c)

Shingo-kikuba

d)

Mkono-wanja

20.

Ndugu na dada wa kike na wa kiume huitanaje?

a)

umbu

b)

mkoi

c)

mpwa

d)

shemeji

21.

Tumia kiulizi kinachostahili.

Mbuzi ______waliochinjwa?

a)

ngapi

b)

zingapi

c)

mangapi

d)

wangapi

22.

Taja neno jingine lenye maana sawa na barua.

a)

mabarua

b)

mtandao

c)

anwani

d)

waraka

23.

Chagua sentensi iliyotumia kiwakilishi cha nafsi.

a)

Wengine wamekamilisha kazi.

b)

Huyu anapenda kuhifadhi mazingira.

c)

Wangu amekamilisha kazi yake.

d)

Sisi tunapenda kula mboga na matunda.

24.

Wakati baina ya saa sita na saa tisa huitwa________

a)

adhuhuri

b)

alasiri

c)

alfajiri

d)

machweo

25.

Sentensi ifuatayo inapatikana katika hali gani?

Mama angeenda sokoni angenunua matunda.

a)

Masharti

b)

Timilifu

c)

mazoea

d)

uliopita

26.

Nomino gani zinazopatikana katika ngeli moja?

a)

chupa, chungu, chakula

b)

saa, dawa, meza

c)

kioo,kitabu,kipofu

d)

mkono,mvua,mkeka

27.

Maneno yaliyopigiwa mstari ni mfano wa aina gani ya maneno.

Kijana aliweka vitabu ndani ya mkoba.

a)

vihisishi

b)

vihusishi

c)

viwakilishi

d)

viunganishi

28.

Jaza pengo kwa alama ya uakifishaji ifaayo.

Mercy alienda dukani kununua___sukari, chumvi, maziwa na mkate.

a)

;

b)

:

c)

'

d)

,

29.

Ni sentensi gani iliyoakifishwa kwa kutumia ritifaa?

a)

Ninayajua matunda mengi:machungwa, mananasi, maembe na maparachichi.

b)

Ng'ombe ni mnyama mwenye faida sana.

c)

Lo! Mvua imenyesha tangu asubuhi hadi jioni.

d)

Ukimaliza kazi umwambie mwalimu wako.

30.

Tumeketi hapa________ saa mbili asubuhi mpaka sasa.

a)

hadi

b)

tangu

c)

mpaka

d)

asubuhi

31.

Tutaendelea kusoma kwa bidii ______tufanye mtihani wa KPSEA.

a)

tangu

b)

hadi

c)

sasa

d)

kuanzia

32.

Ikiwa leo ni Alhamisi,siku ya Jumapili itakuwa________

a)

keshokutwa

b)

mtondogoo

c)

mtondo

d)

juzi

33.

Machache ni kwa mengi kama vile laini ni kwa ____

a)

ngumu

b)

nyembamba

c)

ndefu

d)

nzito

34.

Chagua sentensi yenye nominoambata.

a)

Clarisa aliimba wimbo mzuri.

b)

Ukarimu unafaa katika jamii

c)

Quiana alinunua batamzinga.

d)

Mutie anapenda asali.

35.

Kanusha.

Ukienda uwanjani utampata mchezaji huko.

a)

Usipoenda uwanjani hutampata mchezaji huko.

b)

Ungeenda uwanjani hutampata mchezaji huko.

c)

Ungalienda uwanjani hutampata mchezaji huko.

d)

Ukienda uwanjani hutampata mchezaji huko.

36.

Dada yake mama nitamwitaje?

a)

shangazi

b)

halati

c)

amu

d)

binamu

37.

Mtoto wa ndugu au dada yako anaitwaje?

a)

mkoi

b)

ami

c)

mpwa

d)

wifi

38.

Kamilisha methali.

Achanikaye kwenye mpini ______________.

a)

ndivyo akuavyo

b)

sharti ainame

c)

si mkulima

d)

hafi njaa

39.

Chagua jibu ambalo lina maneno ambayo si visawe.

a)

tabasamu-nuna

b)

rafiki-sahibu

c)

mbogo-nyati

d)

redio-mwengoya

40.

Estelle alipiga miguu hadi nyumbani. Maneno yaliyopigiwa mstari ni mfano wa_______

a)

sitiara

b)

methali

c)

nahau

d)

tashbihi

41.

Andika kinyume cha sentensi hii.

Kijana mrefu amesimama.

a)

msichana mfupi ameketi

b)

kijana mfupi ameketi

c)

mzee mrefu amesimama

d)

mzee mfupi ameketi

42.

Pendo na Zawadi waliagana kwa kusema alamsiki. Huo ulikuwa wakati gani?

a)

asubuhi

b)

adhuhuri

c)

usiku

d)

mchana

43.

Andika kwa wingi.

Ndizi hiyo imeiva vizuri.

a)

Mandizi hayo yameiva vizuri.

b)

Ndizi hayo yameiva vizuri.

c)

Ndizi hizo zimeiva vizuri.

d)

Mandizi hizo zimeiva vizuri.

44.

Chagua jibu lenye maana sahihi ya nahau.

a)

piga hatua-angalia mbele ili usuianguke.

b)

piga hodi- subiri mlangoni ili kufunguliwa

c)

fanya haki- kumpa mtu anachostahili kupata.

d)

fanya bidii- endelea na shughuli fulani kwa kasi

45.

Ni sentensi ipi iliyo katika hali ya udogo?

a)

Kiota cha ndege kinavutia.

b)

Kijito hicho kina maji safi.

c)

Kiberiti kimenunuliwa na mama.

d)

Kiwiko cha mkono wake kimepona.

46.

Chagua jibu linalounganisha sentensi hizi kwa usahihi.

  1. 1. Trina alimpikia Serita chai.

  2. 2. Serita alimpikia Trina chai.

a)

Trina alipikiwa chai kwa Serita.

b)

Serita alipikia chai kwa Trina.

c)

Trina na Serita walipikiana chai.

d)

Serita na Trina walipikiwa chai.

47.

Ni saa ngapi?

a)

Saa tatu kasorobo

b)

Saa tatu na robo

c)

Saa tatu na nusu

d)

Saa tatu kamili

48.

Badala ya sabalheri, ni maamkuzi gani pia tunaweza kutumia?

a)

Salaam aleikum

b)

Cheichei

c)

Chewa

d)

Shikamoo

49.

Chagua neno baki .

a)

Chumvi

b)

chuma

c)

chakula

d)

chandarua

50.

Sanai alipewa shilingi elfu ishirini na wazazi wake ili aazishe biashara.Pesa alizopewa sanai huitwaje?

a)

faida

b)

ushuru

c)

mtaji

d)

riba