Search Header Logo
MSAMIATI WA MAHAKAMANI

MSAMIATI WA MAHAKAMANI

Assessment

Presentation

World Languages

6th - 11th Grade

Hard

Created by

Yaddar Abisai

Used 1+ times

FREE Resource

20 Slides • 0 Questions

1

MSAMIATI WA MAHAKAMANI

Na bwana Yaddar Abisai

2

Pingu/vikuku

Hivi ni vitu vilivyotengenezwa kwa chuma ambavyo hutumiwa kumfungia mshukiwa mikononi ili asitoroke

3

​Dungu

​Mahali ndani ya mahakama ambapo jaji au hakimu huketi wakati wa kusikiliza na kuamua kesi.

4

​Kiongozi wa mashtaka

​Mtaalamu ambaye huendeleza kesi mahakamani. Hueleza kuhusu kesi, mshtakiwa, mshtaki au mashahidi

5

​Karani wa korti

​Mwenye kazi ya kuandika na kutunza nyaraka za korti. Pia hufanya kazi ya kuwaapisha wanaozungumza kortini. (Mshtaki, Mshtakiwa na shahidi)

6

​Ahirisha kesi

​Kitendo cha kusongeza kesi ili isikilizwe wakati mwingine. Jaji au hakimu ndiye mwenye uwezo wa kuahirisha kesi.

7

​Kukata kesi

​Kitendo cha kuamua kesi. Ni jaji tu au hakimu anayeweza kukata kesi.

8

​Korokoroni

​Mahali ambapo mshukiwa hufungiwa ili afikishwe mahakamani. Pia huweza kuitwa kizuizi au seli.

9

​Mahakama au Korti

​Hili jengo ambalo limeundwa spesheli kwa ajili ya mambo ya kisheria.

​(Ngeli ya I-ZI)

10

​Mahakamani/Kortini

​Hapa ni mahali ambapo kesi husikilizwa na kuamuliwa.

​(Ngeli ya pa-ku-mu)

11

​Hakimu / Jaji

​Huyu ni mwanasheria ambaye husikiliza na kuamua kesi mahakamani

12

​Wakili

​Mwanasheria ambaye huwakilisha mshtakiwa, mlalamishi au shahidi mahakamani wakati wa kusikiliza kesi.

13

​Mshukiwa

​Mtu ambaye amekamatwa na askari kwa dai la kutenda uhalifu au kuvunja sheria

14

​Mshtakiwa/mtuhumiwa

​Ni mtu ambaye ameshtakiwa kwa dai la kutenda uovu au kuvunja sheria. Ameshtakiwa na kufikishwa mahakamani

15

​Mshtaki/mlalamishi

​Mtu ambaye huenda kortni kudai kuwa amekosewa au kuvunjiwa sheria.

Mshtaki ni kinyume cha mshtakiwa.

16

​Shahidi

​Anayefika Kortini au mahakamani kutoa habari ambazo zinahusiana na kutendeka kwa kosa au kesi. Shahidi hutoa ushahidi.

17

​Ithibati

​Ni vitu ambavyo hutumiwa mahakamani kuonyesha ukweli wa mambo fulani yanayohusu kesi.

18

​Kizimba

​Mahali ndani ya mahakama ambapo mshtakiwa, mshtaki au shahidi husimama anapotoa taarifa yake kuhusu kesi.

19

​Rumande

​Mahali kule gerezani, ambako mshtakiwa huzuiliwa kesi yake inapoendelea

20

​Dhamana

​Malipo anayolipa mshtakiwa ili awachiliwe huru kesi yake inapoendelea. Mshtakiwa hulipa dhamana ili asipelekwe katika rumande

MSAMIATI WA MAHAKAMANI

Na bwana Yaddar Abisai

Show answer

Auto Play

Slide 1 / 20

SLIDE